BWANA SIMBA, THE KING OF JUNGLE! Simba kwa kiingereza anafahamika kama lion na jina lake la kisayansi (scientific name) anafahamika kama panthera leo na koo(Genus) yake ni panthera, hii koo panthera inajumuisha na wanyama wengine ikiwemo tiger wa bara la asia, chui, American jaguar, na mnyama anaefahamika kama puma au mountain lion. Simba yupo kwenye order ya wanyama walaji wa nyama almaarufu carnivore na familly yake inaitwa felidae, hii familly ya felidae inajumuisha paka wote wanaopatikana duniani ikiwemo wanaofugwa manyumbani, paka pori, simba, chui, tiger, jaguar na wengineo jamii ya paka ikiwemo cheetah (Duma). Simba ndiye paka mkubwa Africa na anashika namba mbili duniani baada ya tiger ambaye anapatikana barani Asia pekee dunia nzima na simba pekee ambaye huishi katika makundi miongoni mwa wanyama jamii ya paka na kundi lao linaitwa (pride) pia simba ni wanyama wanaopendelea kuishi maeneo wazi yenye nyasi(Open area) kama ngorongoro crater na Serengeti national...