Wataalamu waeleza athari za kula chakula katika sinia moja.7 Mei 2019 Sambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Twitter Sambaza habari Zama za mababu na bibi zetu barani Afrika lilikuwa si jambo geni kwa jamii kula chakula katika sahani moja , mfano ugali ukiisha iva, unabwagwa katika sinia moja, bakuli ya mboga ni moja na tena huwekwa katikati ya ugali huo na familia kulizunguka sinia hilo na kila mmoja kula kwa pamoja. Mlo wa pamoja namna hiyo awali ulitafsiriwa kama njia ya kudumisha umoja, mshikamano na upendo lakini pia kama njia ya kumfundisha mtoto ama hata kumrekebisha mkubwa namna anavyo chota tonge, anavyotafuta ili asije akaiaibisha familia mbele za watu , ingawa kadri mabadiliko ya dunia tunamoishi utamaduni huu unadumishwa na wachache . kama hiyo haitoshi,, ikumbukwe kwamba katika baadhi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini bakuli ya kunawia mikono kabla ya kula ilikuwa ni moja tu, na kil...
Maoni
Chapisha Maoni